MISA-TAN YATOA MAFUNZO UHURU WA KUJIELEZA KWA WANAHABARI

Marko Gideon akitoa mafunzo ya uhuru wa kujieleza kwa Wanahabari yaliyo ratibiwa na Misa-Tan.

Na Marco Maduhu, SINGIDA

WANAHABARI wapatao 40 kutoka Mikoa ya Tabora, Dodoma, Shinyanga, Simiyu na Singida, wamepewa mafunzo ya kuandika habari za kukuza uhuru wa kujieleza.

Mafunzo hayo yameanza kutolewa leo Novemba 3, 2022 mkoani Singida ambayo yatachukua muda wa siku tatu ,yakiratibiwa na Taasisi ya vyombo vya habari kusini mwa Afrika tawi la Tanzania( Misa-Tan) kwa ufadhili wa ubalozi wa Kanada nchini Tanzania.

Mwezeshaji wa mafunzo hayo Marko Gideon, amesema mafunzo hayo yametolewa mara baada ya kufanyika utafiti na kubainika kuwa habari za uhuru wa kujieleza hapa nchini zimekosekana.

"Unapokosekana uhuru wa kujieleza, utawala wa Sheria hautakuwepo, uwajibikaji wa viongozi, hakutakuwa na usawa wa kisheria, hakuna uwazi, uchaguzi hauwezi kuwa huru na haki, na kudhibiti matumizi mabaya ya viongozi," amesema Gideon.

Naye Andrew Marawiti kutoka Misa-Tan amesema baada ya mafunzo hayo wanatarajia kuona wanahabari wakiandika habari nyingi zinazohusu uhuru wa kujieleza.

Nao baadhi ya wanahabari walioshiriki mafunzo hayo, wamesema wanatarajia mafunzo hayo kuwaongezea maarifa wakati wa utekelezaji wa majukumu ya uandishi wa habari.

Marko Gideon akitoa mafunzo ya uhuru wa kujieleza kwa wana habari yaliyo ratibiwa na Misa-Tan.

Andrew Marawiti kutoka Misa- Tan akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Andrew Marawiti kutoka Misa- Tan akizungumza kwenye mafunzo hayo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mafunzo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments