AUAWA KWA KUPIGWA RISASI MAJAMBAZI WAKIDHANI KABEBA BEGI LA PESA


Mwanaume mmoja huko Donholm nchini Kenya amefariki dunia baada ya majambazi kumpiga risasi mara nne, na kumpokonya begi waliofikiri lina pesa, ila kupata limejaa vikombe vya karatasi.

Nicodemus Munyasya mwenye umri wa miaka 38, alikuwa ametoka kwenye benki kupeleka hundi, wakati wanaume wawili waliojihami walimfuata kwa kutumia boda boda na kumpiga risasi.

Kwa mujibu wa ripoti kwenye jarida la the Daily Nation, polisi wanashuku kwamba majambazi hao walikuwa wanamjua mwendazake, wakati alipomshambulia eneo la Savannah na kumuitisha begi hilo.

"Alikuwa amebeba begi la mizigo lililokuwa na vikombe vya karatasi, wakati majambazi hao walipodhania zilikuwa ni pesa,” taarifa ya polisi ilisema.

Munyaswa alipigwa risasi mara tatu mguuni na mara moja kwenye kifua. Mwili wake umepelekwa kuhifadhiwa katika chumba cha maiti kwenye Hospitali ya Mama Lucy.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments