RAIS SAMIA AFANYA MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amemteua Innocent Bashungwa, aliyekuwa Waziri wa TAMISEMI kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.


Pia amemteua Dkt. Stergomena Lawrence Tax kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, ambaye amechukua nafasi ya Balozi Liberata Mulamula.

Aidha amemteua Angellah Jasmine Kairuki, kuwa Mbunge na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments