SIMBA SC YAENDELEA KUFANYA VIZURI KIMATAIFA, YAICHAPA 3-1 PRIMEIRO DE AGOSTO


NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba imefanikiwa kuinyuka timu ya Primeiro de Agosto Fc kwa mabao 3-1 mchezo ambao ulipigwa kwenye nchini Angola hivyo nakuwa na faida kwa Simba ambaye atasubiri kucheza mchezo wa marudiano ili aweze kufuzu hatua ya makundi.

Simba Sc iimepata mabao kupitia kwa wachezaji wake Clautos Chama, Israel Mwenda pamoja na mshambuliaji wao hatari Moses Phiri.

Simba Sc ilianza kupata bao la kwanza dakika za mwanzo kipindi cha kwanza kupitia kwa kiungo wao Chama na kuwapeleka mapumziko wakiwa mbele kwa bao 1-0.

Bao la timu ya Primeiro de Agosto Fc lilifungwa dakika za lala salama kupitia kwa mkwaju wa penati.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments