PROF.MWANDOSYA ATEMBELEA DIT

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Prof Mark Mwandosya akitazama mfumo wa gari unaotumia gesi asili mara baada ya kutembelea Taasisi ya teknolojia Dar es Salaam (DIT) leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Prof Mark Mwandosya akioneshwa baadhi ya vifaa vinavyotumika katika kutengeneza mfumo wa gari kutumia gesi asilia mara baada ya kutembelea Taasisi ya teknolojia Dar es Salaam (DIT) leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Prof Mark Mwandosya akizungumza na watumishi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) mara baada ya kutembelea Taasisi hiyo leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Prof. Preksedis Ndomba akizungumza na kumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Prof Mark Mwandosya mara baada ya kutembelea Taasisi hiyo leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Prof Mark Mwandosya (katikati) akiwa pamoja na Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Prof. Preksedis Ndomba baada ya leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam

***************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Prof Mark Mwandosya amezitaka Taasisi za Teknolojia nchini zimetakiwa kuendeleza na kuibua bunifu mbalimbali ambazo zitaweza kuimarisha amendelea ya miundombinu ya kiuchumi nchini.

Akizungumza mara baada ya kutembelea DIT leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam Prof. Mwandosya amesema nchi kama India na nchi nyingine zilizoendelea zimekuwa zikitumia sayansi na teknolojia katika kuwainua vijana na kupambana na umasikini na kupelekea kukua kiuchumi kwa kiasi kikubwa.

Amesema taifa likiwekeza kwenye Taasisi za teknolojia nchini tunaweza kufiika mbali na kuweza kushindana na wenzetu ambao mpaka sasa wameendelea kutokana na kuwekeza kwa muda mrefu kwenye sayansi na teknolojia.

Amesema uhusiano kati ya EWURA na DIT usiishie kwenye gesi bali waendelee kushirikiana kwenye masuala mbalimbali ambayo yatasaidia kulipelekea taifa mbele kiuchumi.

Pamoja na hayo Prof.Mwandosya ameipongeza DIT kwa kuhakikisha wanafanikiwa kubuni na kutengeneza mfumo wa magari kutumia gesi asilia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments