POLISI WAZUNGUMZIA TUKIO LA KATIBU WA KANISA LA MASANJA MKANDAMIZAJI KUJIUA "...ALIKUWA ANAOMBA, ANAMTAKA KIMAPENZI"


Mchungaji Masanja pamoja na Mke wake Monica

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam lisema uchunguzi wa awali wa Polisi kuhusu tukio la Katibu wa Kanisa la Feel Free linaoongozwa na Mchungaji, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ kujiua kwa kujinyonga umeonesha kwamba marehemu, pamoja na mke wa Masanja hawakuwa na mahusiano ya kimapenzi.


Hayo yamebainishwa leo Jumanne, Oktoba 4, 2022 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar, Muliro Jumanne wakati akieleza kuhusu uchunguzi wa jeshi hilo kufuatia tukio hilo ambalo limeibua hisia tofauti kwa wananchi.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne

“Ni kweli uchunguzi wa awali unaonesha mawasiliano yanaonesha huyo marehemu akiwa anaomba, akiwa anataka, anaomba mahusiano ya kimapenzi na huyu, tu ambaye inadaiwa ni mke wa Masanja.

“Ni kweli pia kabla ya tukio mke wa Masanja akiwa na mama mwingine walikwenda nyumbani kwa Marehemu kumueleza kwamba yule Mke hataki msg za namna ile na hataki mahusiano na yeye.


“Ni kweli pia yule mtu alifadhaika baada ya kuelezwa waziwazi kwamba yule ni mke wa mtu na hataki mahusiano nae, sasa mtitiriko wa visa hivyo unatoa nafasi ya kutokuwa na shaka na mazingira ya kifo kile.


“Bila shaka atakua amejinyonga kwa sababu mbalimbali za fikra zake au sababu nyingine yoyote lakini hata hivyo bado Jeshi la Polisi haliwezi likaishia kwenye ushahidi wa awali ambao umeonekana…. mwisho huwa ni kufanya uchunguzi wa kitaalamu,” amesema Kamanda Muliro.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments