Breaking : MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA IGUNGA FATUMA OMARY LATU AFARIKI KWENYE AJALI


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Fatuma Omary Latu na dereva wake amefariki dunia leo katika ajali iliyotokea katika eneo la Shamwengo, Inyala mkoani Mbeya.

Ajali hiyo imetokea leo Septemba 14, 2022, ambapo Mkurugenzi huyo alikuwa anatoka kwenye mkutano mkuu wa 36 wa Jumuiya ya Tawala za Serikali za Mitaa (ALAT), uliofanyika jijini Mbeya.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa chanzo cha ajali hiyo, ni uzembe wa dereva wa gari la mkurugenzi aliyekaidi amri ya jeshi la polisi kusimama ili kupisha msafara wa malori.


Ajali hiyo imehusisha pia magari mengine mawili, likiwemo lori la kubebea mafuta, mali ya kampuni ya Lake Oil na lori lingine la mizigo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Igunga mkoani Tabora, aliyefariki dunia

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments