TANZANIA NJIA PANDA KUFUZU CHAN 2023, YACHAPWA NA UGANDA 1-0


Na Alex Sonna

TIMU ya Taifa Stars imejiweka njia panda kufuzu Michuani ya Wachezaji wa ndani (CHAN) mashindano yatakayofanyika nchini Algeria 2023 baada ya kuchapwa bao 1-0 na Uganda mchezo uliopigwa katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Akitokea benchi Mshambuliaji Travis Mutyaba aliwanyamazisha Watanzania waliohudhuria mechi hiyo dakika ya 87 baada ya kuchachafya ngome ya Taifa Stars.

Tanzania inahitaji kwenda kupindua meza mnamo tarehe 3 Septembar mwaka huu katika uwanja wa St.Mary nchini Uganda timu hizo zitarudiana

Mechi hiyo pia imehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi pamoja Balozi wa Marekani nchini Donald Wright.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments