AKAMATWA NA FUVU LA BINADAMU KIGOMA


Kamanda wa Polisi Kigoma ACP Felomon Makungu
 **
Jeshi la polisi mkoani Kigoma linamshikilia mtu mmoja anayejulikana kwa jina la Taimu Kaogoma mkazi wa Kijiji cha Gwanupu wilayani Kakonko mkoani humo kwa Tuhuma za kukutwa na viungo vinavyodhaniwa kuwa ni vya binadamu ikiwemo fuvu la kichwa na mfupa wa taya.


Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa Kamanda wa Polisi Kigoma ACP Felomon Makungu amesema mtuhumiwa huyo mwenye umri wa miaka 39 alikamatwa Agosti 25 mwaka huu.

Aidha Kamanda Filemon amesema aina hiyo ya matukio imekuwa ikijirudia mkoani Kigoma kutokana na kuwepo kwa baadhi ya watu wanaoamini kufanikiwa kupitia imani za kishirikana na hivyo akawataka wakazi hao kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ili kudhibiti vitendo hivyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments