AZUA GUMZO BAADA YA KUFANYA MAZISHI YA KUMKEJELI MKEWE ALIYE HAI


Mwanaume mmoja katika kijiji cha Emakhwale, kaunti ya Kakamega nchini Kenya amewaacha wakazi wa eneo hilo na mshangao baada ya kufanya mazishi ya kejeli ya mkewe waliyeachana naye.

Jack Shiundu, 32 na mkewe Lydia Masakwe, walinunua kipande cha ardhi mwaka mmoja uliopita na walikuwa wakiishi pamoja.

Shiundu anadaiwa kuchimba shimo na kufukia jeneza hilo dogo na kulifunika kwa nguo na picha za mkewe Masakwe ambaye bado yuko hai. 

Kulingana na TV47, jeneza hilo liligunduliwa na mkulima mmoja.

Alipoichimba, pia alipata kile kilichoonekana kama vipande vya nywele za binadamu ndani ya jeneza.

 Hata hivyo, familia ya Masakwe sasa imewataka polisi kumkamata mshukiwa mbaye ameingia mafichoni.

 Katika kisa cha awali  tuliliripoti kwamba polisi katika kaunti ya Embu wanachunguza kisa ambapo mzee wa miaka 70 anadaiwa kumdunga kisu mkewe hadi kufa baada ya kutofautiana kuhusu KSh 6000. Marehemu mwenye umri wa miaka 42, aliripotiwa kutoweka na pesa walizolipwa baada ya kuuza mbuzi.

Akithibitisha kisa hicho, kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Embu Mashariki Benjamin Muhia alisema baada ya kutoweka, mwanamke huyo alirejea nyumbani akiwa mlevi bila senti hata moja.

 Chifu wa kijiji cha Thau Daniel Ndwiga alisema alipata taarifa ya tukio hilo mwendo wa saa kumi na mbili jioni na alipofika eneo la tukio aliwakuta majirani waliokuwa na hasira wakipanga kumuua mshukiwa.

 Majirani wa wanandoa hao walisema walikuwa na mizozo ya nara kwa mara na hata wiki jana walikuwa na kesi katika fisi ya chifu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments