JAMAA ALIYEKAMATWA NA CHUCHU ZA BINADAMU, NYETI 5 ZA WANAWAKE AFIKISHWA MAHAKAMANI

 


Mkazi wa Maswa, mkoani Simiyu, Salum Nkonja maarufu kama Emmanuel Nkonja, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka 11 yakiwemo kukutwa na chuchu za binadamu, sehemu za siri tano za wanawake na mafuvu mawili ya kichwa cha binadamu.


Nkonja amefikishwa mahakamani hapo leo, Juni 21, 2022 na kusomewa kesi ya uhujumu uchumi namba 32/2022 na wakili wa Serikali, Caroline Materu, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Ramadhani Rugemalira.

Chanzo - Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments