YANGA SC YALAZIMISHWA SARE 1-1 MBELE YA BIASHARA UNITED, YABAKIZA POINTI 3 WATANGAZWE MABINGWA



***************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Yanga imelazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya timu ya Biashara United ya Mkoani Mara kwenye mchezo wa ligi kuu NBC uliochezwa katika dimba la CCM Kirumba Jijini Mwanza.

Mechi hiyo ambayo ilikuwa ya aina yake maana mikikimikiki iliyokuwa ni yakutosha hasa kwa upande wa Yanga ambao walionekana kuwa mwiba dhidi ya wapinzani wao Biashara United kwenye mchezo huo.

Yanga Sc imejaribu kutengeneza nafasi nyingi za wazi lakini wachezaji wao hasa washambuliaji hawakuwa makini kumalizia mipira ambayo ilikuwa inatengenezwa na viungo wao wa pembeni.

Fiston Kalala Mayele anaendelea kuonesha uwezo wake wa upachikaji wa mabao baada ya leo hii kufunga bao kali ambalo lilimshinda kipa wa Biashara United na kutinga moja kwa moja wavuni.

dakika chache tu baada ya Mayele kupachika bao mnamo dakika ya 74 ya mchezo, Biashara nao wakasawazisha bao na kuwafanya waambulia pointi moja kwenye mchezo huo.

Kwasasa Mayele atakuwa na mabao 14 sawa na George Mpole mchezaji wa Geita Gold katika kinyang'anyiro cha ufungaji bora wa ligi hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments