JAMAA AMBAYE HAJASOMEA UFUNDI AUNDA GARI


Ochieng hakuwahi kusomea ufundi wa magari
***

Kipaji ni kitu ambacho watu wengi wamejaliwa kuwa nacho ila ni watu wachache huwa wanafanikiwa kugundua vipaji vyao nakuvifanyia kazi mpaka wanafanikiwa.

Kijana mmoja kutoka Kaunti ya Homa Bay nchini Kenya anayetambulika kwa jina la Bernard Otieno Ochieng, ameshangaza watu kutokana na kipaji chake na uwezo wa ubunifu baada ya kubuni gari lake la siti mbili za kukaa.

Mwaka 2010, Ochieng aliacha shule baada ya kushindwa kulipa karo, baada ya hapo alianza kujifunza ufundi wa magari kwa sababu ni kitu ambacho alikuwa anakipenda tangu akiwa shule.

 Kipindi yupo shule alikuwa anapenda kutumia computer kuangalia mtandaoni jinsi magari yanavyoundwa na kujifunza.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments