AJALI YAUA WATU 8 KUJERUHI 19 NJOMBE




Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Hamis Issah
**
Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Hamis Issah amethibitisha kutokea kwa vifo vya watu 8 na 19 kujeruhiwa katika ajali ya gari aina ya Coaster T 287 CCY mali ya kanisa Katholiki Njombe iliyogongana na lori la makaa ya mawe.

Watu hao ni miongoni mwa Umoja wa vijana kanisa katoliki Jimbo la Njombe (UVIKANJO) ambao walikwenda kuwatembelea watoto yatima katika kituo cha Ibumila wilayani Njombe.

Orodha ya majina ya waliofariki kwenye ajali

Ajali ilitokea jana majira ya jioni katika eneo la Igima wilayani Wanging’ombe Barabara kuu (TANROADS) kuelekea mkoa wa Ruvuma.



Aidha amesema majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya mji wa Njombe Kibena pamoja na hospitali ya rufaa ya mkoa huo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments