Dkt. GWAJIMA AKUTANA NA WAATHIRIKA WA UKATILI WA KIJINSIA SHINYANGA..."TUTASIKILIZA KERO SUGU NCHI NZIMA"


Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima, akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Jasinta Mboneko pamoja na Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mwajina Lipinga, wakisikiliza baadhi ya Waathirika wa matukio ya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto waliojitokeza kufuatia wito wa Waziri huyo jana Aprili 23,2022 akizungumza na kituo cha Redio Faraja mkoani Shinyanga.

Waziri Dkt. Gwajima yupo mkoani Shinyanga kukagua shughuli mbalimbali za Wizara hiyo ikiwepo kuona juhudi za vita dhidi ya ukatili wa kijinsia hususani afua zinazotumika kukabiliana vitendo hivyo.

Mpango huu wa kusikiliza kero sugu za jamii dhidi ya ukatili wa kijinsia na ukatili wa watoto utaendelea katika ziara zake zote nchini.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments