BILIONEA NAMBA 1 DUNIANI ATANGAZA KITITA KIZITO KUINUNUA TWITTER


Bilionea namba moja Duniani Elon Musk

BILIONEA namba moja Duniani Elon Musk ametoa ofa ya Dola Bilioni 43.4 kununua mtandao wa kijamii wa Twitter.

Kwa mujibu wa CNN Business inadai Musk ametuma ofa hiyo ili kumiliki hisa ambazo hazimiliki kwa sasa zenye thamani ya kiasi cha dola 54.20 kwa kila hisa.

Elon Musk ametuma ofa ya Dola Bilioni 43.4 kuinunua Twitter

Musk amesema kiasi hicho cha ofa aliyotoa ndiyo ofa bora na ya mwisho kutoka kwake na kwa mujibu wa SEC ni kwamba Musk alidai ofa hiyo isipokubaliwa basi ataangalia upya nafasi yake kama mwekezaji kwenye Kampuni hiyo.

Twitter ipo njiani kununuliwa na Elon Musk

Mkurugenzi huyo wa Kampuni ya Tesla alinukuliwa akisema:

“Naamini kwamba Kampuni inabidi imilikiwe ili kuweza kupitia mabadiliko mbalimbali ambayo yanatakiwa yafanyike.”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments