MAMA AFARIKI BAADA YA POLISI KUMPOKONYA POCHI YAKE

Scolastica Marada enzi za uhai wake
**
Familia moja katika kaunti ya Trans Nzoia inaomboleza kufuatia kifo cha jamaa yao kilichotokea baada ya afisa wa polisi kuripotiwa kumpokonya pochi lake lililokuwa na KSh 30,000 sawa na shilingi Laki sita za Tanzania.

Scolastica Marada, mama wa watoto watano, alizirai na kufariki baada ya maafisa kutoka Kituo cha Polisi cha Kiminini kuvamia nyumba yake na kupora pesa zilizokusanywa kutoka kwa chama.

 Marehemu alikuwa mfanyabiashara wa chang'aa. 

Kwa mujibu wa Daily Nation, siku hiyo ya mauti, marehemu aliripotiwa kukataa kuwapa polisi hongo ya KSh 1,000 kama 'ada za ulinzi', na kumchochea mmoja wao kumpokonya pochi lake.

"Kwa hiyo mmoja wa askari alinyakua mkoba uliokuwa na pesa ambazo dada yangu alipokea kutoka kwa kikundi chake cha merry-go-round kabla ya kuondoka nyumbani," dada mdogo wa Scolastica, aliyejulikana kwa jina la Brenda, alidai. 

Kulingana na dada yake Emily Nekesa, marehemu mwenye umri wa miaka 36, alikuwa akiugua ugonjwa wa moyo, na alipoanguka, alikimbizwa katika kituo cha afya kilicho karibu lakini akatangazwa kuwa amefariki alipofika “Nilipoingia ndani ya nyumba hiyo, nilimkuta dada yangu akiwa katika hali mbaya akiwa amelala chini, mara moja niliwataarifu majirani zetu waliosaidia kutoa huduma ya kwanza, tukamkimbiza katika Kituo cha Afya cha Solona kwa ajili ya matibabu,” alisimulia. 

Kulingana na Nekesa, dadake alipata fahamu akiwa njiani kuelekea kituo cha afya na kusema kuwa mmoja wa maafisa waliokuwa wamevalia miwani ‘alimuua’ kwa kuchukua pesa zake. "Macho nne amenimaliza, macho nne amebeba pesa zangu elfu thelathini nimepata kwa muganda, macho nne leo ameniua," alisema marehemu.

Chanzo - Tuko News

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments