NDEGE KUBWA ZAIDI YA ABIRIA DUNIANI YAPASUA ANGA SAA TATU IKITUMIA MAFUTA YA KUPIKIA

Ndege ya Airbus A380, imekamilisha safari ya majaribio ya kutumia mafuta ya kupikia kusafiri.

Ndege hiyo ya majaribio ilikamilisha safari ya saa tatu kutoka Uwanja wa Ndege wa Blagnac huko Toulouse hadi makao makuu ya Airbus ya Ufaransa mnamo Machi 25.

 Iliendeshwa na mafuta aina ya Sustainable Aviation Fuel au SAF ambayo mara nyingi hutengenezwa kwa mafuta ya kupikia yaliyotumika na takataka na inafanya kazi kwa injini moja ya Rolls-Royce Trent 900.

Airbus kisha ikafuatisha safari ya pili ya A380, ikitumia mafuta yale yale ya kupikia, mnamo Machi 29, ikiruka kutoka Toulouse hadi Nice. Ndege ya pili ilikuwa kufuatilia matumizi ya SAF wakati wa kupaa na kutua.

Mafuta yaliyotumika yalitolewa na TotalEnergies, kampuni iliyoko katika eneo la Normandy nchini Ufaransa. Airbus imekuwa ikifanya majaribio ya matumizi ya safari za ndege zinazotumia SAF kwa kipindi cha mwaka mmoja, huku A350 ikijaribiwa Machi 2021, na ndege ya njia moja ya A319neo ikiruka kutumia mafuta ya kupikia mnamo Oktoba. Kampuni hiyo inatarajia kupata kibali cha ndege yake kuruka kwenye SAF ifikapo mwishoni mwa muongo huu.

Hivi sasa, ndege za Airbus zinaweza kuendeshwa na hadi 50% ya SAF, iliyochanganywa na mafuta ya taa ya asili. Kampuni hiyo inadai kuwa ndege zinazoruka kwenye SAF zinaweza kufikia kati ya 53% hadi 71% ya upunguzaji wa kaboni unaohitajika kufikia lengo hilo. Airbus inapanga kuzindua ndege ya kwanza duniani isiyotoa hewa chafu sokoni ifikapo mwaka wa 2035. Ndege kubwa zaidi ya abiria duniani za A380 imekuwa ikipungua katika miaka ya hivi karibuni huku mashirika kadhaa ya ndege yakitaka kumalizwa kwa muda wa matumizi yao, kwa misingi ya utumizi wa mafuta ikilinganishwa na ndege za kisasa za masafa marefu.

Airbus iliwasilisha ndege ya mwisho ya A380 kwa shirika la ndege la Dubai Emirates mwishoni mwa 2021.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments