SERIKALI YAANZA MCHAKATO KITAMBULISHO CHA NIDA KITUMIKE KUPIGIA KURA

Serikali ya Tanzania imesema imeanza mchakato wa kuunganisha kitambulisho cha Taifa na kitambulisho cha mpiga kura ili kumfanya mtanzania kutumia kitambulisho cha taifa katika zoezi la kupiga kura.

Akiuliza swali bungeni leo Mbunge wa Kawe Askofu Josephat Gwajima alitaka kujua kama Serikali haioni umuhimu wa kuunganisha mifumo ya Kitambulisho cha Mpiga Kura na Kitambulisho cha Taifa ili kuepusha usumbufu kwa Wananchi,

Akijibu swali hilo kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Hamis Hamis amesema serikali imeanza mchakato wa kuunganisha vitambulisho hivyo viwili na kufanya sasa mtanzania kutumia kitambulisho cha taifa katika mchakato wa Uchaguzi wa kawaida na ule wa kieletroniki ‘e-voting’.

Naibu Waziri Hamis amesema kuwa matumizi hayo yatapunguza gharama kwa Serikali katika kuandikisha na kutengeneza daftari pamoja na kurahisisha usimamizi wa wapiga kura.

Ameeleza kuwa Mawasiliano kati ya Taasisi hizo mbili yenye dhumuni la kuiwezesha Kanzidata ya NIDA kutumika katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura yameanza mwezi Machi, 2022.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments