BABA AMUUA MTOTO WAKE KWA SHOKA AKIGOMBANA NA MKEWE




Jeshi la Polisi mkoani Kagera linamshikilia mwanaume aitwaye Anderson Clemence (35), mkazi wa kijiji cha Kafunjo, Kata ya Kamagambo wilayani Karagwe kwa tuhuma za kumuua mtoto wake Hansen Anderson, mwenye umri wa miezi minne kwa shoka.


Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Wankyo Nyigesa, amesema kuwa baba huyo alikamatwa Machi 01, 2022 na kwamba chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi baina yake na mke wake.

Amesema kuwa wakati wakigombana mtuhumiwa alirusha shoka ili kumpiga mke wake na badala yake likampiga mtoto huyo aliyekuwa amebebwa mgongoni na mama yake mzazi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments