AUAWA KWA KUKANYAGWA NA TEMBO AKITAFUTA KUNI NGORONGORO


Tembo

Mfugaji aitwaye Narudwasha Titika, mkazi wa kijiji cha Alaitore kilichopo ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, amefariki dunia jana Machi 9, 2022, majira ya saa 7:00 mchana baada ya kushambuliwa na Tembo sehemu mbalimbali za mwili wake, wakati akitafuta kuni.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha ACP Justine Masejo, na kusema kwamba uchunguzi wa awali wa jeshi hilo umebaini kuwa marehemu alikutwa na mkasa huo wakati akitafuta kuni akiwa na wenzake ndani ya hifadhi hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post