TMA YATOA ANGALIZO LA MVUA KUBWA NA UPEPO MKALI




Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa angalizo kwa wananchi juu ya hali ya hewa katika siku kadhaa zijazo.

ANGALIZO la mvua kubwa limetolewa kwa maeneo machache ya mikoa ya Morogoro, Iringa, Njombe, Songwe, Mbeya, Ruvuma Lindi na Mtwara.
UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI.


KIWANGO CHA ATHARI ZINAZOWEZA KUTOKEA: WASTANI.

JUMATATU 07-02-2022

ANGALIZO la mvua kubwa limetolewa kwa maeneo machache ya mikoa ya Dodoma, Morogoro, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe, Rukwa, Ruvuma Lindi na Mtwara.

ANGALIZO la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2.0 limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya bahari ya Hindi mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Dar es Salaam na Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia) pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI.
KIWANGO CHA ATHARI ZINAZOWEZA KUTOKEA: WASTANI.

JUMANNE 08-02-2022

ANGALIZO la mvua kubwa limetolewa kwa maeneo machache ya mikoa ya Morogoro, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Lindi na Mtwara.



ANGALIZO la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2.0 limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya bahari ya Hindi mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Dar es Salaam na Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia) pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI.
KIWANGO CHA ATHARI ZINAZOWEZA KUTOKEA: WASTANI.



JUMATANO 09-02-2022
ANGALIZO la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2.0 limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya bahari ya Hindi (mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Dar es Salaam na Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia) pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba).
UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI.

Utabiri huu umetolewa,
Na, MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments