SIMBA SC YATOA DOZI YA KIBABE KOMBE LA SHIRIKISHO, YAICHAPA ASEC MIMOSAS 3-1


*************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Simba Sc imefanikiwa kuondoka na alama tatu kwenye kombe la Shirikisho hatua ya makundi mara baada ya kuichapa ASEC Mimosas ya nchini Ivory Coast kwa mabao 3-1.

Simba Sc ilianza kupata bao la kwanza dakika ya 12 ya mchezo kupitia kwa kiungo wao Mshambuliaji raia wa Senegal Papa Sakho akifunga bao tamu na kuwanyanyua mashabiki ambao walikuwa wanashuhudia mechi hiyo kabambe.

Kipindi cha kwanza kiliisha huku Simba ikiwa kifua mbele kwa bao 1-0, kipindi cha pili klabu ya ASEC Mimosas iliendelea kupambana kuweza kusawazisha bao kwenye mchezo huo kwa kufanya mashambulizi mengi na kufanikiwa kusawazisha bao kupitia kwa Stephane Aziz Ki.

Licha ya ASEC Mimosas kusawazisha Simba Sc nao katika harakati za kushambulia kipa wa ASEC Mimosas alimchezea rafu Yusufu Mhilu na refa kuamuru ipigwe penati ambayo ilikwenda kupigwa na Shomari Kapombe na kufanya matokeo kuwa 2-1.

Bao hilo lilidumu kwa dakika mbili tu za mchezo kabla ya Kiungo Mshambuliaji raia wa Malawi Peter Banda kugongelea msumari wa mwisho na kufanya matokeo kuwa 3-0 Simba ikiondoka na alama tatu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments