WATUMISHI MSAJILI WA HAZINA WABORESHA AFYA KWA MICHEZO


Michael Mzoo (wa kwanza kulia) akiwaongoza Watumishi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina katika mchezo wa kuvuta kamba wakati wa Bonanza Maalumu la Michezo lililofanyika jana katika Viwanja vya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Jijini Dar es Salaam.

(Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Pili Mazowea akizungumza na Watumishi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wakati wa Bonanza Maalumu la Michezo lililofanyika jana katika Viwanja vya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Jijini Dar es Salaam.

(Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Pili Mazowea (Kushoto) akifurahia ushindi pamoja na washindi wa Mpira wa Mguu wakati wa Bonanza Maalumu la Michezo lililofanyika jana katika Viwanja vya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Jijini Dar es Salaam.

(Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Pili Mazowea (Kushoto) akikabidhi tuzo ya mshindi wa pili wa mbio fupi upande wa wanawake kwa Neema Matagi wakati wa Bonanza Maalumu la Michezo lililofanyika jana katika Viwanja vya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Jijini Dar es Salaam.

(Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Pili Mazowea (Kushoto) akikabidhi tuzo ya mshindi wa mbio fupi upande wa wanaume kwa Felix Ngoi, wakati wa Bonanza Maalumu la Michezo lililofanyika jana katika Viwanja vya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Jijini Dar es Salaam.

(Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Pili Mazowea (Kulia) akipokea tuzo kama shukrani kutoka kwa Irene Minja (Kushoto) akiwakilisha watumishi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wakati wa Bonanza Maalumu la Michezo lililofanyika jana katika Viwanja vya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Jijini Dar es Salaam.

(Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Pili Mazowea (Kushoto) akikabidhi tuzo ya mshindi wa pili katika mbio za magunia upande wa wanawake kwa Avelina Rwilemera, wakati wa Bonanza Maalumu la Michezo lililofanyika jana katika Viwanja vya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Jijini Dar es Salaam.

(Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Pili Mazowea (Kushoto) akikabidhi tuzo ya mshindi wa pili katika mbio za magunia upande wa wanaume kwa Peter Maungo, wakati wa Bonanza Maalumu la Michezo lililofanyika jana katika Viwanja vya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Jijini Dar es Salaam.

(Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)

*********************

Na Mwandishi Maalumu

KATIKA kuhakikisha watumishi wake wanakuwa na afya bora na kuboresha mahusiano mahali pa kazi, Ofisi ya Msajili wa Hazina jana ilifanya Bonanza kubwa kwa ajili ya watumishi wake lililofanyika Viwanja vya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Jijini Dar es Salaam.

Zaidi ya wanamichezo 100 walifurahia Bonanza hilo lililoshirikisha mazoezi ya viungo, mpira wa miguu, kuvuta kamba, riadha, mbio za magunia na kukimbiza kuku.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha bonanza hilo, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Pili Mazowea aliyekuwa mgeni rasmi akimwakilisha Msajili wa Hazina, Mgonya Benedicto, alisema lengo kuu la Bonanza hilo ni kuimarisha afya ya watumishi na kuboresha mahusiano mahali pa kazi.

Aliongeza kuwa, afya ikiwa nzuri kwa watumishi hata utendaji kazi unakuwa mzuri, hivyo amewasihi kushiriki michezo mara kwa mara ili kuimarisha afya.

Aliwapongeza pia watumishi walioshiriki katika bonanza hilo kwa kujitokeza kwa wingi, akiamini watakuwa mabalozi wazuri kwa wengine katika kutunza afya zao kupitia michezo.

Washindi wa michezo mbalimbali walizawadiwa vikombe huku washiriki wakitunukiwa medali.

Hilo lilikuwa bonanza la pili kwa watumishi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina kufanyika kati ya mwaka jana na mwaka huu na kwanza aina hiyo ya kusanyiko la kimichezo litakuwa endelevu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments