MAMA ASHTUKA KUTAMBUA KUWA MUME WAKE NI NDUGU YAKE WALIYEZAA WATOTO WATATU


Domitila alizaliwa mnamo mwaka 1978, lakini mwaka mmoja baadaye mama yake alifariki dunia.

Kisha miaka michache baadaye alimpoteza baba yake na hivyo alikuwa na ndugu wengi ambao walikulia katika familia tofauti.

Katu hakuwa anamfahamu kaka yake japo jamaa zake walikuwa wakimuarifu kwamba ana kaka.


Baada ya miaka mingi, Domitila alianza kufanya kazi kama kijakazi na siku moja alikutana na kaka yake jijini Kigali, Rwanda, lakini hawakujua wao ni watu wa damu moja.

Jane Mugo: Kizaazaa Kortini Huku Mpelelezi Binafsi Akiangua Kilio, Adai Watekaji Nyara Walikuwa Wakimfuata
Waoana
Ndugu hao walipendana sana na kisha walioana na kujaliwa watoto watatu.

Baadaye waligundua kwamba wao ni ndugu wa damu moja waliotoka tumbo moja na baba yao ni mmoja.

Taarifa hiyo ilimdunisha Domitila na kumfanya kujidharau sana akijifungia akijificha kukutana na watu.

"Nilichanganyikiwa na kuanza kujificha kwa watu. Niliacha hata kuchota maji..." alisema katika mahojiano na AfriMax.

Domitila alisema watu walikuwa wamdhihaki pamoja na wanawe wakisema walizaliwa na damu moja na hivyo kumlazimu kutengana na kaka yake.

Mama huyo anaishi katika nyumba mbovu ambayo haijamalizwa kujengwa na hapokei msaada wowote kutoka kwa baba ya watoto wake.

Kifungua mimba wa Domitilia na mwanawe wa pili wana matatizo tofauti za kiafya.

Domitila alisema ni miaka mitano sasa tangu atengane na kaka yake ambaye hataki kujihusisha na wanao.

Anawaomba wasamaria mema kumsaidia kujenga nyumba mpya kwa ajili ya familia yake na kuwapeleka watoto wake shuleni.

Jamaa ashtuka kutambua anachumbiana na mke wa kakake
Jamaa Atekwa Nyara Dakika Chache Baada ya Kuondolewa Gerezani Wajir

Katika kisa sawia na hicho, TUKO.co.ke, iliripotia kumhusu mwanamume Mkenya mwenye miaka 36, ambaye alishtuka kutambua amekuwa katika mahusiano ya mapenzi mke wa kaka yake mdogo.


Katika mahojiano ya kipekee na mhariri wa mahusiano wa TUKO.co.ke, Gitau alifichua kwamba amekuwa kwenye ndoa kwa miaka mitatu na ana hisia ya mapenzi kwa wanawake na wanaume ingawa mkewe hajui.

Baba huyo wa watoto wawili alifichua kwamba alikutana na mpenzi wake wa jinsia moja kwenye programu ya uchumba ya Tinder mnamo 2020 na alishtuka kugundua alikuwa ni mke wa kaka yake wakati wa hafla ya familia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments