BUNDI ATUA KANISANI..AIMBA KWAYA KWA MARINGO KAMA BINADAMU, TAZAMA HAPA


Video maridadi inayomuonyesha Ndege aina ya bundi,akiwatumbuiza waumini kanisani katika taifa la Jamhuri ya Dominika imewachangamsha wengi.

Bundi huyo  aliwaacha waumini vinywa wazi pamoja na wanamtandao baada ya kuonekana kanisani wakati wa ibada.

Huku wanakwaya hao wakiwatumbuiza waumini na nyimbo tamu, bundi huyo anaonyeshwa akiwa katika paa la kanisa akisakata densi kama inavyoonyeshwa kwenye video iliyopakiwa na @nowthisnews kwenye Instagram.

"Bundi huyu anaonekana kuwa na wakati mzuri wa kucheza muziki wa injili katika kanisa moja la Jamhuri ya Dominika," video hiyo ilinukuu.

Waumini wa kanisa hilo katika Jamhuri ya Dominika, walisema bundi huyo alicheza nyimbo hizo zote kwa saa moja.


Kwa mshangao wa wengi, bundi huyo alionekana kufurahishwa na wimbo wa wanakwaya waliokuwa wakiwatumbuiza waumini

Huku baadhi ya wanamtandao wakihusisha ndege huyo na uchawi, wengine walisema kuwa wimbo wa kwaya ulikuwa wa kupendeza na kuwaondolea ndege 'bahati mbaya'

@kitschykatz: "Inapendeza sana, siwezi! Mungu ni mzuri sana! Na kiumbe huyu ananitoa machozi!"

@dai_dreaming_ : "Huyo ni mtu ambaye amefariki hivi karibuni na anawatembelea tu!"

@joanflakes "Walifikiri ni mchawi (imani iliyozoeleka katika nchi za Amerika Kusini)."

@myartisindie: "Ndio, ningekuwa nikifanya vivyo hivyo, mara tu baada ya kisanduku cha mpigo kuwashwa."

@callmemisterj: "Bila shaka bundi alikuwa. Mungu, Wadominika na Jamhuri ya Dominika wote ni wa ajabu."

@mrckly: "Nilifikiri walisema ni mchawi na walikuwa wakijaribu kuitisha, lol." abn_ghozt210: Ninaiona kuwa ya kupendeza, lakini katika Amerika ya Kusini na Mexico hii inaweza kuwa roho au ishara mbaya."

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

1/Post a Comment/Comments

Post a Comment