BoT YAELEZEA BAADHI YA MAJUKUMU YA KURUGENZI YA MASOKO YA FEDHA

 

Fidelis Mkatte Mchambuzi wa Masuala ya Fedha Katika Benki Kuu ya Tanzania BoT wakati akitoa mada kwa waandishi waandamizi na wahariri wa vyombo mbalimbali nchini katika semina inayofanyika kwa siku 5 kwenye Tawi la benki hiyo jijini Mbeya.

Bi. Vick Msina Kaimu Meneja wa Uhusiano na Itifaki Benki Kuu ya Tanzania (BoT) akifafanua jambo kabla ya kuanza majadiliano mara baada ya wasilisho la  mada kwa waandishi waandamizi na wahariri wa vyombo mbalimbali nchini katika semina inayofanyika kwa siku 5 kwenye Tawi la benki hiyo jijini Mbeya.

.......................................

Majukumu ya Kurugenzi ya Masoko ya Fedha katika Benki Kuu ya Tanzania BoT ni Kusimamia na kuendesha soko la dhamana za serikali ambapo  Kurugenzi huendesha minada ya Dhamana za Serikali ili Kudhibiti ujazi wa fedha unaosababisha mfumuko wa bei na kuainisha mwelekeo wa riba katika soko la fedha.

Hayo yameelezwa leo na Fidelis Mkatte Mchambuzi wa Masuala ya Fedha  Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakati akitoa mada kwa waandishi waandamizi na wahariri wa vyombo mbalimbali nchini katika semina inayofanyika kwa siku 5 kwenye Tawi la benki hiyo jijini Mbeya.

 Amesema majukumu mengine ya kurugenzi hiyo  ni kuiwezesha serikali kukopa kwa ajili ya shughuli mbali mbali za maendeleo ili kuziba nakisi ya bajeti ya matumizi ya kawaida ya serikali katika utendaji wa majukumu yake ya utekelezaji wa maendeleo na shughuli za kawaida za serikali.

Sambamba na hilo, Kurugenzi hiyo ni msimamizi wa Soko la Ndani la Fedha - Inter-bank Cash Market (IBCM). Pamoja na usimamizi wa minada, Kurugenzi husimamia pia soko la jumla la fedha za kigeni (Interbank Foreign Exchange Market (IFEM).. 

"Jambo lingine kubwa ni kutekeleza sera ya uangalizi wa thamani ya shilingi na Kuleta utulivu katika soko (Orderly Market) ambapo pia Benki Kuu hushiriki katika soko hilo sambamba na benki za biashara ili kuimarisha na kuilinda thamani ya shilingi yetu  na Usimamizi wa Akiba ya Fedha za Kigeni," Amesema Fidelis Mkatte.

Aidha amebainisha kuwa Kurugenzi pia  inawajibika kusimamia akiba ya fedha za kigeni kwa mujibu wa sera ya fedha za kigeni na sheria ya Benki Kuu ya mwaka 2006 na Kuhakikisha kuwa kuna kiasi cha kutosha ikiwa ni pamoja na kuiwezesha serikali kulipia kwa wakati mahitaji mbali mbali kama vile Deni la taifa

Ameongeza kuwa kazi nyingine ya Kurugenzi hiyoni kuwekeza katika taasisi salama na kwenye amana zilizo salama ili kulinda thamani na usalama wa akiba yenyewe (“Capital preservation”), Usimamizi wa Akiba ya Fedha za Kigeni na utunzaji na Uwekezaji wa Fedha za Kigeni Nchi za Nje

Ameongeza kuwa Benki Kuu ndiyo yenye dhamana ya kutunza hazina ya fedha za kigeni za nchi kwa niaba ya Serikali kwa kuziwekeza katika mabenki na taasisi mbalimbali za fedha nje kwa faida. ambapo Benki Kuu ina Sera na Mwongozo (“Reserve Management Policy and Guidelines”) zinatoa mwongozo wa utunzaji wa fedha za kigeni ikiwa ni pamoja na Usimamizi wa Akiba ya Fedha za Kigeni, Utunzaji na Uwekezaji wa Fedha za Kigeni Nchi za Nje.

Amefafanua kuwa jukumu lingine ni  uamuzi wa wapi pa kuwekeza au taasisi gani ya kuwekeza ambapo Benki Kuu huzingatia zaidi usalama wa fedha hizo za kigeni sambamba na jukumu hilo, Benki Kuu hutumia hazina hiyo ya fedha  kufanya malipo mbalimbali ya nje kutokana na majukumu mbalimbali yanayoikabili Serikali.

Bi. Vick Msina Kaimu Meneja wa Uhusiano na Itifaki Benki Kuu ya Tanzania BoT akifafanua jambo kabla ya kuanza majadiliano mara baada ya wasilisho la  mada kwa waandishi waandamizi na wahariri wa vyombo mbalimbali nchini katika semina inayofanyika kwa siku 5 kwenye Tawi la benki hiyo jijini Mbeya.

Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mada kuhusu Majukumu ya Kurugenzi ya Masoko ya Fedha  katika semina ya waandishi wa habari inayofanyika katika tawi la (BoT) jijini Mbeya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments