BINTI WA MIAKA 17 AJIUA KWA CHANDARUA BAADA YA KUACHIKA MARA TATU



Mwanamke aliyetambulika kwa jina la Rebecca Benjamin, Mkazi wa Kata ya Izunya, Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita, mwenye umri wa miaka 17, amefariki dunia kwa kujinyonga kwa kile kinachoelezwa kuwa ni msongo wa mawazo baada ya kuolewa na kuachika mara tatu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amesema mwanamke huyo alikutwa amejinyonga kwa kujining’iniza kwenye kenchi la nyumba aliyokuwa anaishi kwa kutumia kamba iliyosokotwa kwa chandarua kutokana na msongo wa mawazo.

Kamanda Mwaibambe ameyasema hayo alipokutana na kamati ya amani na maadili ya Mkoa wa Geita uliokuwa na lengo la kutokomeza matukio ya watu kuua na kujiua.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments