WABUNGE WA TANZANIA WAITWA BUNGENI SAA CHACHE BAADA YA SPIKA NDUGAI KUJIUZULU


Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Nenelwa Mwihambi leo Ijumaa, Januari 7, 2022 amesema baada ya Job Ndugai kujiuzulu nafasi ya Uspika kwa sasa taratibu za uchaguzi wa kujaza nafasi hiyo zinaendelea na kwamba kwa mujibu wa sheria kiti cha Spika kinapokuwa wazi hakuna shughuli yoyote itakayotekelezwa katika Bunge isipokuwa Uchaguzi wa Spika.

Katika taarifa yake, Mwihambi amesema Kamati zilizokuwa zikutane kianzia Januari 10, 2022 na Januari 17, 2022 hazitokutana kwa wakati huo na badala yake zitakutana wakati wa Mkutano wa Sita wa Bunge Februari 1-11, 2022 kwa utaratibu wa tarehe zitakazotangazwa na hivyo Wabunge wameombwa kufika Dodoma Januari 31, 2022.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments