JAMAA AWEKA MABANGO KUTAFUTA MKE



Mwanaume mmoja ambaye hajaoa anatumia mabango makubwa yenye ujumbe mwingi-ndani katika harakati zake za kupata mke.

Muhammad Malik, 29, anawaarifu washirika watarajiwa kuhusu upatikanaji wake na mabango ya matangazo London na Birmingham.


Yalisema: "Niokoe kutoka kwa ndoa iliyopangwa."

Alisema hayuko kinyume na dhana hiyo lakini angependelea kujaribu "kutafuta mtu peke yangu kwanza".

Marafiki wa Muhammad Malik walimsaidia kutengeneza mabango ili kupata mke

Lakini hadi sasa msako huo umethibitisha kutozaa matunda kwa mshauri huyo wa benki mwenye makazi yake London ambaye anatumai kuwa tovuti maalum - findmalikawife.com - itabadilisha bahati yake.

Tangu aandike matangazo siku ya Jumamosi, Bw Malik anasema amekuwa na mamia ya jumbe zinazoonyesha nia


"Sijapata wakati wa kuangalia bado," alisema. "Ninahitaji kuweka muda kando - sikuwa nimefikiria sehemu hii."


Ndani ya siku chache, Bw Malik alisema alikuwa amepokea mamia ya jumbe

Bw Malik alisema alijaribu njia kadhaa za kukutana na wanawake kabla ya kutumia mabango.

"Mimi ni Desi wa Kipakistani," alisema, "kwa hivyo jambo la kwanza tunaloambiwa ni nguvu za shangazi." Lakini njia hiyo "haikufaulu".

Kisha kulikuwa na programu za uchumba na matukio machache ya uchumba, lakini alisema yalimwacha akijihisi "mchanganyiko kabisa".

Hatimaye, rafiki yake alipendekeza ajitangaze kihalisi. Bw Malik alieleza: "Nilifikiri 'kwanini - ni nini kibaya zaidi kinachoweza kutokea'?"

Mabango hayo, ambayo yamepangwa kubaki hadi Januari 14, yanaungwa mkono na familia, huku wazazi wake wakiwa naye kwa hilo "tangu mwanzo", ingawa alikiri: "Ilinibidi kumshawishi mama yangu kidogo."


Bw Malik alisema mchumba wake ajaye bora awe muislamu

Chanzo - BBC Swahili

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments