Tazama Picha : JINSI MOTO ULIVYOTEKETEZA SOKO LA KARUME DAR ...RC MAKALLA ATAKA WAHANGA WATAFUTIWE ENEO

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla,amewaomba wahanga wa moto Soko la Karume kuwa watulivu, kwani inaundwa kamati ya kuchunguza chanzo cha moto katika Soko la Karume ambapo vyombo vyote ya ulinzi na usalama pamoja na Afisa Biashara Jiji na mkoa wataingia kwenye kamati hiyo.

Makalla ameyasema hayo leo Januari 16, 2022 baada ya kufika eneo la Karume Ilala Jijini Dar es salaam kujionea hali ya Soko la Karume ambalo limeteketea kwa moto alfajiri ya leo.

''Serikali itafanya jitihada ya kuhakikisha kwamba tunajua chanzo lakini pia tunakuja na suluhisho ya sisi kurejea katika kufanya biashara baada ya kupokea taarifa na maamuzi ya nini kifanyike katika soko hili,'' ameeleza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla.

''Tuwaombe muwe watulivu. Majanga haya yanapotokea yanahitaji maneno ya faraja kama ambayo tunawapa, lazima tutafute njia mbadala ili maisha yaendelee," amesema Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla.

''Si rahisi leo ukadhani kwamba baada ya hapa tutaacha tu kamati ifanye kazi, watu hawa walioko hapa lazima maisha yaendelee na ili maisha yaendelee ni maelekezo yangu kwamba Uongozi wa Jiji la Dar ukiongozwa na DC na Uongozi wa Soko, tuangalie namna ambavyo tunaweza kuwasaidia Wafanyabiashara hawa katika masoko ya jirani,'' ameongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla.
Baadhi ya Wafanyabiashara katika Soko la Bidhaa za Mitumba la Karume Mchikichini, Ilala Dar es salaam wakijaribu kutafuta vitu watakavyoweza kuokoa bila mafanikio kufuatia soko hilo kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo Jumapili Januari 16,2022.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments