AJALI YA TRENI YAJERUHI NA KUSABABISHA KIFO CHA MTOTO TANGA



Shirika la Reli Tanzania (TRC) limetoa taarifa kuwa Treni ya abiria yenye injini namba 9022 imepata ajali majira ya saa 10 Alfajiri kati ya Mkalamo na Mvave Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga January 16,2022 ikiwa inatokea Arusha kuelekea Dar es salaam ikiwa na behewa 14 zenye abiria 700 ambapo behewa 5 zilipinduka na nyingine 4 ziliacha njia na kupelekea majeruhi watano na kifo cha Mtoto mmoja mwenye umri wa miaka saba.

Shirika la Reli limesema linaendelea kufuatilia kwa ukaribu kufahamu chanzo cha ajali hiyo ili kuchukua hatua.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments