MTANGAZAJI MAARUFU WA REDIO AJIUA STUDIO


Mtangazaji maarufu na mpakuaji muziki (DJ) wa kituo cha redio cha Capital FM Alex Nderi almaarufu DJ Lithium ameaga dunia.

Kwa mujibu wa ripoti kadhaa za vyombo vya habari, mpakuaji miziki huyo alijiua kwa kunywa sumu katika afisi za kituo hicho jijini Nairobi.

 Wafanyakazi wenzake wanasemekana kumpata akiwa amepoteza fahamu dakika chache baada ya kubugia kemikali hiyo. 

Waliitisha msaada mara moja, juhudi zao za kumwamsha zikiambulia patupu na hivyo kumkimbiza katika Hospitali ya Nairobi

. Madaktari walimshughulikia lakini wakashindwa kumwamsha ikiwa dhahiri kuwa alikuwa ameondoka duniani. 

Nderi anadaiwa kufuta peji zake katika mitandao ya kijamii kabla ya kujitoa uhai huku pia akiacha barua ambayo wafanyakazi wenzake wamefichua kuwa itafunguliwa tu na jamaa zake.

Kisa hicho kimethibitishwa na Kamanda wa kituo cha polisi cha Kilimani MuturiMbogo ambaye vilevile amedokeza kuwa Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) imezamia suala hilo. 

Mbogo amesema kuwa mwili wake umepelekwa katika hifadhi ya maiti ya Lee ambako upasuaji utafanywa kubaini chanzo cha kifo hicho.

 Visa vya watu kujitia kitanzani vimeongezeka nchini huku wito wa kuangazia afya ya akili ya wakenya ukitolewa.

 Kwa mujibu wa takwimu za Huduma ya Kitaifa ya Poliis (NPS) wa zaidi ya watu 500 walijitoa uhai katika miezi sita ya mwanzo ya mwaka 2021. Frank Njenga, mshauri wa rais kuhusu afya ya akili, alithibitisha takwimu hizo na kuongeza kuwa idadi hiyo imeongezeka pakubwa huenda kutokana na athari za janga la Korona.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments