Post Top Ad
Friday, January 21, 2022
MIILI YA WANAWAKE WATATU WALIOUAWA NA KUTUPWA JIJINI MWANZA YAZIKWA
Miili ya watu watatu wa familia moja waliouawa jijini Mwanza imezikwa mjini Sengerema leo Januari 21,2022.
Akiongoza ibada ya maziko nyumbani kwa marehemu Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Imakulata Bomani mjini humo, Padri Fred Mgabi amesema waliofanya mauaji hayo hawana hofu ya Mungu na hawajawahi kufika kanisani na kwamba hukumu yao wataikuta kwa Mungu kutoka na matendo yao.
Tukio la wanawake watatu kuuawa kikatili kisha miili yao kutupwa, lililotokea Januari 19, 2021 katika Mtaa wa Mecco Kusini, Kata ya Mecco jijini Mwanza.
Waliouawa ni Mary Charles, Janeth Fred pamoja na Monica Jonas na miili yao ilipowasili wananchi waliangua vilio kutokana na mauaji yaliyofanywa na watu wasiojulikana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Malunde 1 blog ni blog ya Kiswahili maarufu duniani kwa habari za Matukio, Siasa, Magazeti, Nyimbo za asili na habari za kusisimua.
No comments:
Post a Comment