YANGA YATINGA RAUNDI YA NNE KOMBE LA FA , YAICHAPA IHEFU FC MABAO 4-0


*************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Klabu ya Yanga imefanikiwa kutinga raundi ya nne kombe la shirikisho (FA) mara baada ya kufanikiwa kuwachapa Ihefu Fc mabao 4-0 kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Heritie Makambo ndiye alikuwa mwiba kwa wapinzani katika kipindi cha kwanza alifanikiwa kupachika mabao mawili na bao lingine likifungwa na Khalid Aucho na kwenda mapumziko Yanga ikiwa mbele kwa mabao 3-0.

Kipindi cha pili Yanga ilipinguza kasi ya mchezo mara baada ya kuwapumzisha baadhi ya mastaa wake kadhaa, hivyo baadae Heritie Makambo akapachika tena bao lake la tatu katika mchezo huo na kuiwezesha timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 4-0.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments