WATU WATATU WAFARIKI KWA AJALI YA GARI GEITA


WATU watatu waliokuwa wakisafiri kutoka Kata ya Nzera kuelekea Geita Mjini wakitumia gari la abiria (aina ya Toyota Hiace) wamefariki dunia papo hapo na wengine nane kujeruhiwa baada ya gari lao kugongana na Lori katika eneo la Pori la Mgodi wa GGM Wilayani Geita Mkoani Geita.

Akithibitisha vifo hivyo, Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Geita ambayo ndio imepokea mii ya marehemu hao na kuihifadhi, Dk. Paschal Thumba amesema walipokea miili hiyo ya watu watatu huku wengine wakipewa rufaa ya kupelekwa Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments