RAIS MWINYI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI WALIOFARIKI KWA KULA NYAMA YA KASA




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu waliofariki kufuatia kula samaki wa aina ya kasa anayesadikiwa kuwa na sumu huko Matemwe, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Katika salamu hizo za rambirambi, Rais Dk. Mwinyi ameeleza kusikitishwa na vifo hivyo na kuzinasihi familia za marehemu hao kuwa na subira na ustahamilivu katika kipindi hichi kigumu cha msiba pamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu kuwaponya kwa haraka waliodhurika baada ya kula samaki huyo.



Rais Dk. Mwinyi katika salamu hizo za rambirambi, amesema kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara yake husika itaendelea kuhakikisha wale wote waliodhurika wanaendelea kupatiwa tiba ili waweze kurudi katika hali zao nzuri za kiafya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments