MZAZI AMBURUZA MAHAKAMANI MWANAE .."HANIPI MSAADA..ANAKULA TU STAREHE MJINI'


Mzee Gideon Kisira Cherowo
Mzee Gideon Kisira Cherowo (73) Mkazi wa Bungoma nchini Kenya amemfungulia kesi katika mahakama Kuu ya Kitale Mtoto wake aitwaye Washington Chepkombe akitaka akatwe asilimia 20 ya mshahara wake ili apewe Mzee huyo kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya Familia kwa kuwa Mtoto wake huyo hampi msaada licha ya kuwa na kazi nzuri na fedha nyingi.

Mzee huyo anasema Sasa ni miaka 17 tangu kijana wake aonekane nyumbani na mzee ameamua kufika mahakamani ili kijana ashurutishwe kuwa awe anatuma 20% ya mshahara wake.

Mzee huyo anasema alilazimika kuuza hadi ardhi yake na mali zake nyingine ili kulipia ada za masomo ya Mtoto wake huyo hadi Chuo Kikuu na akafanikiwa kupata kazi kwenye Mamlaka ya Viwanja vya Ndege lakini baada ya kupata kazi hampi msaada.

Mzee huyo amesema ana Watoto wanne lakini mwenye kazi ni Washington pekee na kusema kwa sasa yeye na Familia yake wanaishi katika nyumba ya udongo kijijini kwao huku Mtoto wao mwenye uwezo akila starehe Mjini.


“Nimepambana sana kumtafutia maisha Mtoto ili atusaidie lakini hatupi msaada kwa kuwa mshahara wake ni mzuri nimefungua kesi ili 20% ya mshahara wake nilipwe mimi..”,amesema


Gideon Kisira Cherowo mwenye umri wa miaka 73 alisema mwanae ni mwajiri wa Halmashauri ya Usimamizi wa Viwanja vya Ndege nchini KAA ambapo hupokea mshahara kila mwezi.

 Hata hivyo, alisema mwanawe hajaweka kiwango chochote kuwafikia wazazi wake ambao sasa wamekosa namna kutokana na uzee.

Kisira aliambia mahakama kuwa alifanya kila awezalo ili mwanawe kusoma akijua atakuwa tegemeo kwake siku za uzeeni.

 "Nilitumia mali yangu yote ili kuhakikisha kuwa atakuwa katika nafasi ya kutusaidia. Kwa sasa, mimi na mke wangu tuko katika hali mbaya licha ya kuwa tuna mtoto ambaye yuko kazini. Naomba mahakama iamuru atupe asilimia 20 ya mshahara wake nikiwa kama babake," alisema mzee huyo


Inaarifiwa mwanawe ana miaka 48 na mzee Kisira anasema aliuza hadi shamba lake ili weze kumpa masomo.

"Niliuza shamba langu eneo la Cheptais, Bungoma, na kumsomesha kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu. Nilimpa pia robo ekari. Mimi pia nilimlipia mke wake mahari ambapo ilinigharimu ng'ombe wanne na fedha," Kisira alisema kwenye kesi katika mahakama Kuu ya Kitale. 

Alisema mwanawe alipata kazi na KAA 2008 lakini hajawahi kuwasaidia wazazi wake kwa chochote.

 Aidha aliongeza kuwa kwa miaka 17 sasa hajawahi kufika nyumbani wala kutuma hata sumni nyumbani. 

Sasa anataka mahakama iagize kijana huyo kuwa akituma nyumbani asilimia 20 ya mshahara wake ili wazazi wake wapate riziki. Hata hivyo, kesi hiyo ni ya namna yake kwani hakuan sheria iliyopo kuhusu jinsi watoto wanafaa kusaidia wazazi wao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments