ASTON VILLA YAMTANGAZA GERRARD KUWA KOCHA WAO MPYA


********************* 

NA EMMANUEL MBATILO 

Klabu ya Aston Villa ya nchini Uingereza imemtangaza Steven Gerrard kuwa kocha wao Mkuu kuchukua mikoba ya Dean Smith ambaye alitimuliwa hivi karibuni kutokana na matokeo mabovu. 

Gerrard alikuwa mchezaji wa Liverpool kwa muda mrefu na kupata mafanikio makubwa kwenye klabu hiyo na baadae kustaafu kucheza soka. 

Mwaka 2018 Steven Gerrard alitangazwa kuwa kocha Mkuu wa klabu ya Rangers ya nchini Scotland ambapo kwenye hiyo ameipa mafanikio ikiwemo kushinda taji la ligi hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments