WAZIRI MWAMBE AKAGUA UWEKEZAJI WA KIWANDA KIPYA CHA MBOLEA DODOMA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Uwekezaji , Mhe. Geoffrey Mwambe, leo tarehe 16 Oktoba, 2021, amekagua shughuli za uwekezaji katika Mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha kuzalisha Mbolea asilia cha ITRACOM FERTILIZERS LIMITED, kinachojengwa katika eneo la Nala, jijini Dodoma.

Mradi huo ni miongoni mwa miradi yenye hadhi ya uwekezaji maaluum, ukiwa na mtaji wa Dola za Marekani milioni 180 na unatarajiwa kuzalisha ajira 3000. Aidha, mradi huo utasaidia kuingiza fedha za kigeni, kipato kwa wananchi na mapato ya serikali kupitia kodi

Katika ziara hiyo Mhe. Mwambe ameabatana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka pamoja na Watendaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Dodoma.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments