RAIS SAMIA AAHIDI KUTATUA CHANGAMOTO MBALIMBALI ZINAZOUKABILI MKOA WA KILIMANJARO
Friday, October 15, 2021
Rais Samia Suluhu Hassan amewaahidi wakazi wa wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo kero ya maji, migogoro ya ardhi pamoja na kukamilisha ujenzi wa kilomita 44 za barabara zilizobaki kutoka Elerai hadi Kamwanga.
Rais Samia ameyasema hayo wakati akizindua kipande cha barabara ya Sanya juu- Elerai chenye urefu wa kilomita 32.2 kilichogharimu kiasi cha shilingi bilioni 62.7.
Amesema barabara ya Sanya Juu – Kamwanga ilikuwa ni kero ya siku nyingi kwa wananchi, na hivyo amewataka wananchi kuitunza ili iweze kudumu na kuwa na manufaa kwao na watoto wao.
Awali, akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara ya Sanya Juu – Elerai, Mtendaji Mkuu wa TANROAD, Rogatus Mativila amesema usanifu wa vipande viwili vya Bomang’ombe – Sanya Juu (24km) na Elerai – Kamwanga (44km) umekamilika na ujenzi wake utaanza hivi karibuni.
Mativila amesema ujenzi wa barabara ya Sanya Juu – Elerai ulikamilika April 29,2019 ambapo tayari mkandarasi ameshalipwa kiasi cha shilingi bilioni 45.9.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin