NAIBU WAZIRI MARY MASANJA AFUNGUA KIKAO KAZI KILICHOANDALIWA NA TFS KUHAMASISHA UTALII


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Mary Masanja akizungumza wakati akifungua kikao kazi kilichoandaliwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuhamasisha Utalii nchini. Ufunguzi huo umefanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Mary Masanja akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe.Jokate Mwegelo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kilichoandaliwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuhamasisha Utalii nchini. Ufunguzi huo umefanyika leo Jijini Dar es Salaam.


Kamishna Msaidizi Kamanda wa kanda ya Mashariki Dar es Salaam, Pwani na Morogoro (TFS) Bi.Caroline Malundo akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kilichoandaliwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuhamasisha Utalii nchini. Ufunguzi huo umefanyika leo Jijini Dar es Salaam.Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe.Jokate Mwegelo akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kilichoandaliwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuhamasisha Utalii nchini. Ufunguzi huo umefanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Kamishna Msaidizi-Maendeleo ya ufugaji wa nyuki Bw.Hussein Msuya akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kilichoandaliwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuhamasisha Utalii nchini. Ufunguzi huo umefanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Wasanii, waandishi wa habari na wanamichezo wakifuatilia kikao kazi kilichoandaliwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuhamasisha Utalii nchini. Ufunguzi huo umefanyika leo Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

**************************

NA EMMANUEL MBATILO,DAR ES SALAAM

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Mary Masanja amesema misitu iliyopo nchini ni muhimu kwa shughuli za uchumi wa nchini, na uchumi wa mtu mmoja mmoja.Mchango wa sekta ya misitu ni mkubwa tofauti na inavyoripotiwa kwenye vitabu vya uchumi kuwa ni asilimia 3.5 kwenye pato la Taifa.

Mchango huo unaweza kuongezeka kwa kurasimisha shughuli za misitu zitambuliwe kama vile kukuza viwanda vya kuchakata mazao ya misitu, kurasimisha shughuli za upandaji miti na ujenzi wa viwanda vya kuchakata mazao ya nyuki.

Ameyasema hayo leo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja wakati akifungua kikao kazi kilichoandaliwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuhamasisha Utalii nchini.

Akizungumza mbele ya wasanii, waandishi wa habari na wanamichezo Naibu Waziri wa Mary amesema Tanzania imejaaliwa neema ya kuwa na uoto wa rasilimali za misitu kwa asilimia 55 ya eneo la nchi.

"Eneo hill lina ukubwa wa wa takribani hekta milioni 48 ambazo zipo katika maeneo mbalimbali na kusimamiwa na TFS ikiwemo hifadhi za misitu ya asili, mashamba ya miti, hifadhi za misitu ya mazingira asili, misitu ya mikoko na misitu iliyo kwenye ardhi ya huria

"Hakuna asiyefahamu umuhimu wa rasilimali hizi mlizopewa dhamana ya kusimamia, rasilimali mnazosimamia zina umuhimu mkubwa katika nyanja zote za maisha ya binadamu na viumbe. Kimazingira rasilimali za misitu zinatunzwa bionuiwai na mifumo ikolojia inayowezesha uhai wa viumbe vyote," amesema.

Hivyo amesema bila misitu hakuna wanyamapori na uhai wa binadamu utakuwa hatarini kwani wote wanatumia hewa ya oksijeni inayozalishwa na miti na kwamba kijamii misitu yetu ni muhimu kwa ajili ya shughuli za jadi.

"Hivyo ili kudumisha utamaduni na mila zetu lazima tutunze misitu yetu ambayo ndio hazina ya historia yetu," Amesema.

Aidha, amesema misitu ni muhimu katika shughuli za uchumi wa nchi na uchumi wa mtu mmoja mmoja, na kwamba mazao mbalimbali yanayozalishwa na msituni kama mbao na magogo huchakatwa na kuwa bidhaa za viwandani zinazochangia fedha za kigeni na ajira.

Amesema vyanzo vingi vya maji yanayotumika kwa shughuli za majumbani, mashambani, viwandani na kwenye mabwawa ya kuzalisha umeme ni misitu.

Aidha, shughuli za uanzishaji misitu binafsi kwa njia ya upandaji miti unawezesha mwananchi mmoja mmoja kunufaika na fursa za misitu.

Amefafanua bidhaa za viwandani zinazotokana na mazao ya misitu na ufugaji nyuki zitaongeza ajira na mauzo ya nje,hivyo kuna jukumu kubwa kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kutunzwa na kuendelezwa ili kukidhi majukumu hayo ya kimazingira, kiuchumi na kijamii kwa kuzingatia kizazi cha sasa na kijacho.

"Serikali meweka msisitizo mkubwa katika utekelezaji wa majukumu haya. Leo tuko hapa kwa ajili ya kuzungumzia suala la utalii ikolojia kama zao mojawapo la misitu yetu, shughuli hii katika dhana ya uhifadhi wa misitu ni mpya na inashamiri kwa kiwangi kikubwa".

"Mnafahamu kuwa wizara imepewa jukumu la kuhakikisha idadi ya watalii inaongezeka kufikia watalii milioni tano ifikapo mwaka 2025 na kuongeza mapato yanayotokana utalii kufikia dola za Marekani bilioni sita". Ameeleza.

Hata hivyo amesema utalii unachangia zaidi ya asilimia 17 ya Pato la Taifa na asilimia 25 ya mapato ya fedha za kigeni hivyo mchango huu kwa kiwango kikubwa unachangiwa na wageni wanaotembelea nchini kwa ajili ya utalii wa wanyama.

"Mchango wa utalii utaongezeka kama tutahamasisha na kuimarisha utalii ikolojia na kuhamasisha utalii wa ndani," amesema na kuongeza anafahamu wizara ilikasimu usimamizi wa vituo sita vya malikale kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania .

"Vituo hivyo ni muhimu kwa ajili ya kuendeleza utalii wa malikale na utalii wa utamaduni.Ni muhimu jitihada za uendelezaji na utangazaji wa utalii ikolojia uendelee sambamba na utangazaji wa vituo hivyo ambavyo ni Ngome Korogwe, Kaole, Magofu ya Tongani ,Tembe la Kwihara, Kituo cha Kumbukumbu ya Livingstone na Michoro ya Miamba ya Kolo," amesema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments