MKOA WA SINGIDA WABAINIKA KUWA NA ALMASI BORA TANZANIA

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya JICT LTD inayojishughulisha na Utafiti wa Almasi Javan Bidogo ambaye pia ni mmiliki wa mradi wa utafuta wa Almasi katika Kijiji cha Mbereseke kilichopo Wilaya ya Iramba mkoani hapa, akimuelekeza jambo Naibu Waziri Wizara ya Madini Profesa Shukuru Manya (wa pili kulia mbele) wakati alipofanya ziara yake ya kikazi ya siku moja ya kutembelea na kukagua mradi huo jana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya JICT LTD inayojishughulisha na Utafiti wa Almasi Javan Bidogo ambaye pia ni mmiliki wa mradi wa utafuta wa Almasi katika Kijiji cha Mbereseke kilichopo Wilaya ya Iramba mkoani hapa, akitoa maelezo kwa  Naibu Waziri Wizara ya Madini Profesa Shukuru Manya (katikati) wakati alipofanya ziara yake ya kikazi ya siku moja ya kutembelea na kukagua mradi huo jana.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda akizungumza wakati wa ziara hiyo. Kutoka kushoto ni Naibu Waziri Wizara ya Madini Profesa Shukuru Manya, Kamishna wa Madini Dkt. Abdulrahaman Mwanga, Kaimu Afisa  Madini Mkazi Mkoa wa Singida,Chone Malembo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya JICT LTD inayojishughulisha na Utafiti wa Almasi Javan Bidogo.
Kazi zikiendelea katika mgodi huo.
Naibu Waziri Wizara ya Madini Profesa Shukuru Manya na ujumbe wake wakiangalia udongo ambao unasubiri kuingizwa kwenye mtambo ili kubaini kama una Almasi. 
Kamishna wa Madini Dkt. Abdulrahaman Mwanga, akiangalia mtambo (karasha) wa kusaga mawe yenye Almasi uliopo katika mgodi huo.
Kazi zikiendelea katika mgodi huo.
Muonekano wa sehemu ya mgodi huo.
 



Na Dotto Mwaibale Iramba


MKOA wa Singida umebainika kuwa na Almasi bora zaidi kuliko maeneo yote Tanzania.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya JICT LTD inayojishughulisha na Utafiti wa Almasi Javan Bidogo ambaye pia ni mmiliki wa mradi wa utafuta wa Almasi katika Kijiji cha Mbereseke kilichopo Wilaya ya Iramba mkoani hapa wakati akitoa taarifa ya mradi huo kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Profesa Shukuru Manya alipofanya ziara yake ya kikazi ya siku moja ya kutembelea mradi huo jana.

Bidogo alisema kampuni yao imejikita kufanya utafiti wa Almasi katika wilaya za Ikungi na Iramba tangu mwezi Machi mwaka jana na hatua wanayoendelea nayo ni ya mwisho.

"Tumefanya uvumbuzi katika baadhi ya miamba inayokuwa na Almasi jumla yake ipo 13 na kati ya hiyo tisa ni mikubwa ambayo tumekuwa tukiifatilia sana,". alisema Bidogo.

Bidogo alisema kwa hivi sasa wamechukua sampuri ya udongo na kuanza kuziosha kwenye mtambo wao uliopo kwenye mradi ili waweze kuziona Almasi zote ambazo zipo kwenye udongo huo ambao wameuchukua kutoka maeneo mbalimbali wilayani Ikungi na Iramba.

Alisema mtambo wao ambao wataufunga kwa ajili ya kuanza kuhutumia kuosha mchanga huo wiki mbili zijazo kuanzia sasa una uwezo wa kuosha tani 10 za mchanga huo kwa muda wa saa moja.

Alisema kwa kuanza wanatarajia kuwa na ajira za wafanyakazi wasio pungua 50 kwa muda huu wa kwanza wa utafiti ambao wanaumalizia lakini kadri Mungu atakavyo wasaidia na kuwa na mchanga wenye Almasi watatarajia kuwa na wachimba 1000 kwa kila mgodi mmoja.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo Naibu Waziri Wizara ya Madini Profesa Shukuru Manya alisema Serikali kupitia wizara hiyo sasa ni kitu kimoja kwani inafanya kazi kwa umoja kwa kushirikiana na wadau wengine kama wakuu wa mikoa na wilaya katika maeneo mbalimbali ikiwemo eneo la madini. 

Alisema jambo hilo ni nzuri na ndilo analolisisitiza wakati wote Rais Samia Suluhu kuwa wao waliopewa dhamana ya uongozi wasaidie kufanya uwekezaji kwenye maeneo yao ili uweze kukua.

" Ninyi wenzetu mliopo kwenye nyadhifa za ngazi ya Tamisemi mnapo wiwa kutekeleza masuala haya ya uwekezaji kwa dhati na dhamira ya mioyo yenu na kuwa kama uwekezaji huo ni wenu binafsi kwa ajili ya kuongeza uzalishaji ni jambo zuri na la kutia moyo.

Alisema uchumi wa madini ni tofauti na uchumi wa mazao ambao unahitaji kilo ngapi za pamba kwa kilo moja ya dhahabu hapo  ndipo utakapoweza kujua uwekezaji katika madini jinsi unavyo kuwa na tija ya mapato hadi kwenye Halmashauri za wilaya mbalimbali.

Alisema mafanikio hayo yatapatikana kwa kuzuia migogoro ambayo haina tija katika maeneo mbalimbali yakiwemo ya uchimbaji wa madini.

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda alisema amemshirikisha Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida kuwa wachimbaji wadogo wenye leseni waalikwe ili kufanya mazungumzo nao lengo likiwa na wao wapate maeneo ya kuchimba na wale ambao hawana uwezo wasaidiwe kuwatafuta wawekezaji ambao watashirikiana nao jambo litakaloongeza uzalishaji.

Baadhi ya wataalamu wa miamba katika mgodi huo wakizungumza na waandishi wa habari walisema katika miamba walioifanyia utafiti imeonesha Mkoa wa Singida kuwa na Almasi bora hapa nchini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments