HUYU NDIYE MWANAMKE MREMBO NA MWENYE MVUTO ZAIDI DUNIANI



Mwanamitindo maarufu nchini Marekani, Isabella Khair Hadid “Bellahadid” mwenye asiri ya Palestina na Dutch, anatajwa kuwa ndio mwanamke mrembo zaidi duniani.

Kwa mujibu wa tafiti za wanasayansi wa masuala ya urembo, Bellahadid ambaye aliwahi kushinda taji la Mwanamitindo wa Mwaka (“Model of the Year 2016”) inaelezwa kwamba muonekano wake hauna kasoro kwa asilimia 94.35.

Watafiti hao wamezingatia vitu vifuatavyo katika maumbile ya Bellahadid.

👉PUA
👉MACHO
👉 KOMWE
👉KIDEVU
👉 KICHWA

Uchunguzi uliofanywa na “Golden Ratio of Beauty Phi,” ulieleza kwamba;


“Bella Hadid ni mwanamke mrembo na mwenye mvuto zaidi duniani kwa kuwa na muonekano mzuri. Kila kitu hapa kipo kamili, kuanzia taya, macho, midomo mpaka uso.”

Mpaka sasa tunapozungumza (Mwaka huu 2021), Bellahadid bado anaendelea kushikilia nafasi ya kwanza kwa urembo duniani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments