MBWA MWENYE MASIKIO MAKUBWA ZAIDI AVUNJA REKODI YA DUNIA

 Rekodi ya Dunia ya Guinness imetangaza mshikilizi wa rekodi mpya, na ni mbwa kwa jina Lou na mmiliki wake Paige Olsen kutoka Milwaukee nchini Marekani.

Mbwa  huyo ameingia katika orodha ya Rekodi za Dunia za Guinness kama mbwa mwenye masikio marefu.

Wanamtandao waliduwazwa na mbwa huyo huku wengine wakimzulia matani kuwa mnyama huyo ana uwezo wa kusikia kila kitu kutoka mbali.

Lou kutoka Milwaukee nchini Marekani ana masikio yenye urefu wa inchi 13.38 kila upande.

 Hii ndio kile shirika hilo liliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook:

"Ana masikio yote! Mshikilizi wetu mpya wa mbwa mwenye masikio marefu ni Lou, mbwa mwenye rangu nyeusi na hudhurungi aina ya Coonhound kutoka Milwaukie, Oregon,marekani. Masikio ya Lou yana urefu wa centimita 34 (inchi 13.38 ) yote, kama ilivyoangaziwa kwenye kitabu cha #GWR2022 wiki hii."

She's all ears! Our new record holder for longest ears on a dog is Lou, a black and tan Coonhound from Milwaukie, Oregon, USA. Lou's ears measure an impressive 34 cm (13.38 in) each, as featured in the new #GWR2022 book released this week.

"Lou might think she's special - but I think she's thought that from the beginning," says owner Paige Olsen."I think she's always known she's a little bit better than the rest of us."

"Now people can't wait to get her paw-digraph! I'm very proud of the furry little munchkin for being so special."

9.4K
1K
3.3K

Mmiliki wa mbwa huyo pia alifurahia rekodi hiyo ya swahiba wake akisema:

"Lou anaweza kufikiria ni spesheli lakini nadhani alifikiria hivyo kutokea mwanzo. Nafikiri amekuwa akijihisi kuwa bora kutuliko sisi sote. Sasa watu watakuwa na hamu ya kupiga picha naye. Ninamfurahia sana rafiki yangu mdogo kwa kuwa spesheli."

 Wanamtandao waliduwazwa na mbwa huyo huku wengine wakimzulia matani kuwa mnyama huyo ana uwezo wa kusikia kila kitu kutoka mbali.

 @Sudiksha Kumar alisema: "Natafakari anavyojaribu kula chakula bila kusikia, mbwa huyu anaweza kusikia watu wakifungua switi wakiwa mbali."

@Carmelo Alim Acibar alisema: "Kidogo tu na mbwa huyu atapeperuka."

 @Michelle Barone: :Hauwezi kumficha siri."

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments