MBUNGE WA MASWA MAGHARIBI MASHIMBA NDAKI AZIDI KUTOA MISAADA KWA JAMII



Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi Mhe. Mashimba Ndaki agawa jezi 13 kwa timu za mpira katika jimbo hilo ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa ahadi zake katika kukuza sekta ya michezo katika jimbo hilo na kuwahamasisha vijana kucheza kwa bidii na kuhakikisha wanafikia malengo ya kucheza katika timu kubwa ndani na nje ya nchi.

Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi Mhe. Mashimba Ndaki akiwa kwenye picha ya pamoja na vijana kutoka katika timu 13 za mpira wa miguu baada ya kugawa jezi na mipira katika timu hizo zilizopo katika Jimbo la Maswa Magharibi na kuwataka kuhakikisha jezi na mipira inatumika katika malengo yaliyokusudiwa ya kukuza sekta ya michezo katika jimbo hilo.


Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi Mhe. Mashimba Ndaki akitoa msaada wa magongo ya kutembelea kwa mmoja wa walemavu wa miguu ikiwa ni sehemu ya msaada wake kwa watu wenye mahitaji maalum katika jimbo hilo.


Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi Mhe. Mashimba Ndaki akitoa msaada wa baiskeli maalum kwa ajili ya walemavu wa miguu kwa mmoja wa walemavu ikiwa ni sehemu ya msaada wake kwa watu wenye mahitaji maalum katika jimbo hilo.


Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi Mhe. Mashimba Ndaki akitoa msaada wa fimbo malum ya kumuongoza mlemavu asiyeona ikiwa ni sehemu ya msaada wake kwa watu wenye ulemavu huo katika jimbo lake ikiwa ni muendelezo wa misaada mbalimbali ambayo amekuwa akitoa kwa wenye mahitaji maalum.

Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi Mhe. Mashimba Ndaki akitoa msaada wa fimbo malum ya kumuongoza mlemavu asiyeona ikiwa ni sehemu ya msaada wake kwa watu wenye ulemavu huo katika jimbo lake ikiwa ni muendelezo wa misaada mbalimbali ambayo amekuwa akitoa kwa wenye mahitaji maalum.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments