IGP SIMON SIRRO APANGUA MAKAMANDA WA POLISI




Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Simon Sirro amefanya mabadiliko madogo ya makamanda wa Polisi wa mikoa kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa polisi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa jeshi hilo, David Misime imeeleza kuwa, Kamishna msaidizi wa Polisi, ACP Revocatus Malimi amehamishwa kutoka mkoa wa Kagera kwenda makao Makuu ya Polisi Dodoma.

Aidha,nafasi yake imechukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi, Kamishna Msaidizi waPolisi, ACP Awadhi Juma Haji.

Wakati huo huo, Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Omary Said Nassiri amehamishwa kutoka Makao Makuu ya Polisi Zanzibar na kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments