MAAFISA BIASHARA WATAKIWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO YA MSINGI



Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA ) Bw. Godfrey Nyaisa akifafanua jambo wakati wa ufunguzi wa Mafunzo kwa Maafisa Biashara wa mikoa ya Morogoro, Dodoma na Singida yanayofanyika kwa wa siku tano jijini Dodoma.


Maafisa biashara kutoka mikoa ya Dodoma, Morogoro na Singida wakifuatilia mafunzo ya sheria ya leseni za biashara yanayotolewa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) yanayofanyika katika ukumbi wa JK convetion Centre jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Bw. Godfrey Nyaisa (aliyeketi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Biashara wa mikoa ya Dodoma, Singida na Morogoro mara baada ufunguzi wa mafunzo ya Sheria ya Leseni za Biashara yanayofanyika kwa siku tano katika ukumbi wa JK Convetion Centre Jijini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi wa Leseni wa BRELA Bw. Andrew Mkapa na kutosho kwake ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Leseni wa BRELA, Bw. Tawi Kilumile

**************************

Na mwandishi Wetu, Dodoma





Maafisa biashara nchini wametakiwa kutambua kuwa jukumu lao kuu ni kuwezesha ufanyaji wa biashara badala ya kuwa wakusanya mapatato shughuli ambayo ni sehemu tu ya kazi ambayo wanatakiwa kuifanya.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo ya sheria za leseni za biashara kwa maafisa biashara wa mikoa ya Dodoma, Singida na Morogoro, yanayofanyika jijni Dodoma, Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bw. Godfrey Nyaisa amesema Maafisa Biashara wanapaswa kutumia sheria pia kutumia busara wakati wa utekelezaji wa majukumu yao na kwamba ikiwa watazifunga biashara wasitarajie mfanyabiashara huyo kufanya biashara na badala yake watachangia kuua uchumi wa nchi.

“Muepuke sana kufunga biashara, afisa biashara kazi yako kubwa ni kusimamia wafanyabiashara, ikiwa utaifunga biashara utasimamia watu gani, hii ina maana huwataki wafanyabiashara “, alisema Bw. Nyaisa na kuongeza kuwa anatarajia kuwa mafunzo hayo yatasaidia kubadili fikra na mitizamo ya maafisa biashara na watendaji wengine wa serikali na kuwa watoa huduma na msaada kwa wafanyabiashara, hivyo ni vema wakafuatilia mafunzo hayo vizuri ili watakaporudi katika vituo vyao vya kazi watumike kama chachu ya uwekezaji, ukuaji na uanzishwaji wa biashara.

Bw. Nyaisa amesema, kila mmoja awe kipimo kwa kuwezesha watu kuanzisha na kufanya biashara ili ifikapo mwisho wa mwaka kila mmoja ajipime na kujihoji ni watu wangapi aliowawezesha kuanzisha biashara, wawafuate watu na kuwawezesha kuanzisha biashara na sio watu wawafuate wao kutaka kuanzisha biashara na wasiwe watu wanaokimbiwa na wafanyabiashara.

Sambamba na hilo maafisa biashara hao wametakiwa kutoa huduma bora na kwa weledi jambo ambalo litawezesha wafanyabiashara walio wengi kurasimisha biashara kupata fursa mbalimbali zinazotolewa na serikali ama taasisi mbalimbali za kifedha.



Amesisitiza kuwa maafisa biashara wana jukumu la kuwaelimisha wafanyabiashara kutambua umuhimu wa kusajili biashara zao na kupata leseni pamoja na kufanya ufuatiliaji wa karibu kwa wafanyabiashara hao ili kuendelea kukuza uchumi wa nchi.

Amewataka wafanyabiashara kuondokana na dhana kwamba gharama ya usajili wa majina ya biashara na makampuni kubwa jambo ambali si kweli kwani BRELA ni taasisi ya huduma na gharama zinazotozwa ni ndogo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments