Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Benki ya CRDB, TullyEsther
Mwambapa akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu
Tamasha la Kizimkazi 2021 ambalo lifanyika kuanzia
tarehe 23 hadi 28 mwezi huu. Tamasha hilo litahusisha mafunzo na
maonyesho ya bidhaa za wajasiriamali, maonyesho ya kitamaduni na sanaa,
mchezo wa mpira wa miguu na pete pamoja na michezo ya asili ya
Kizimkazi. Tamasha hilo pia litatumika kukabidhi miradi ya maendeleo ya
Kizimkazi kwa Mgeni Rasmi ambae ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan.Akizungumzia katika mkutano na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Benki ya CRDB, TullyEsther Mwambapa amesema kuwa Lengo la CRDB Bank ni kulifanya tamasha hili kuwa endelevu, lenye kutangaza vivutio mbalimbali vya Zanzibar, kuchochea utunzaji wa mazingira and kutoa fursa za kiuchumi kwa wana Kizimkazi. Kizimkazi ina utajiri mkubwa wa vivutio vya kiutalii ikiwemo fukwe, dolphins, hoteli za Kisasa, tamaduni na historia ya Kizimkazi. Kupitia matangazo yetu mbalimbali mtaona na kusikia hazina kubwa iliyoko Kizimkazi.
Futari hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai pamoja na mawaziri mbalimbali wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania sambamba na Sheikh Mustafa Shaaban, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambae aliiongoza dua ya kuiombea Benki ya CRDB kwa kufuturisha katika kipindi hiki cha mfungo wa Ramadhani.


Social Plugin