FUMANIZI LA HADI UWE NA CHETI CHA NDOA LAZUA GUMZO...WANASHERIA WASHAURI BADALA YA KUFUMANIA WADAI FIDIA TU

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene
**
Wakati mjadala wa sharti la cheti cha ndoa kwenye fumanizi ukishika kasi, imeelezwa kuwa zipo ndoa hazina vyeti na zinatambulika kisheria, lakini wengi hawana uelewa huo.

Hata hivyo, baadhi ya wanasheria wamewashauri watu badala ya kufumania, kufungua kesi ya madai na kumdai fidia kiasi chochote mtu mwenye uhusiano na mwenza wake.

Juzi, Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene alisema, “itahesabiwa fumanizi hadi pale huyo anayefumaniwa, iwe mwanamke au mwanaume awe na cheti cha ndoa halali. Sio mtu alikuwa rafiki yako kwa muda, wewe bado unatafuta uhalali wa kuonekana unammiliki, unamvamia na kurekodi picha kisha kusambaza.”
Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments